HIVI NI KWELI MWENGE WA UHURU UNACHOCHEA MAAMBUKIZI YA UKIMWI? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

HIVI NI KWELI MWENGE WA UHURU UNACHOCHEA MAAMBUKIZI YA UKIMWI?

MTAZAMO WANGU.

Mwenge wa Uhuru licha ya maana yake kuwa nzuri na yenye faida nyingi katika kuleta umoja wa kitaifa, upendo na amani hasa siku hizi ambapo vitu hivyo vimeanza kutoweka, lakini wapo watu au makundi ya watu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiitikadi wamekuwa wakiuponda na kuonyesha kwamba hauna faida yeyote na hata ungefaa ufutiliwe mbali.



Watu wengine hudai kwamba kila panapokuwa na mikesha ya mwenge, asubuhi mahali hapo hukutwa mipira kibao ya kiume imetapakaa, ikiashiria palitendeka vitendo vya kizinzi usiku. Lakini la kujiuliza ni kwamba vitendo hivyo hufanywa na wanyama au binadamu wenye akili na  utashi? .Matendo mabaya ya kizinzi hayachagui mahali pa kufanyiwa ilimradi tu pamekuwa na giza au usiri, kwani hujawahi  kusikia habari za viongozi wa dini kutenda mambo hayo tena ndani ya nyumba za ibada wanapojua hamna mtu anayemuona?

Hakuna nchi duniani isiyokuwa na tunu zake za kitaifa, yapo mambo unaweza ukayaona ya kijinga lakini, umuhimu wake utaujua pale utakapo achana nayo. Wakati Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo Amos Makalla akiwajibu wabunge waliotaka kujulishwa faida za mwenge na bajeti yake kwa mwaka, alisema falsafa yake ni kuwaletea wananchi nuru palipokuwa na giza, kuheshimiwa na kukombolewa.

  
Mbunge wa Simanjiro Ole Sendeka aliomba muongozo akidai Mwenge huo ambao ni alama na tunu ya taifa kuleta tumaini pale ambapo hapana matumaini kwa wale wanaojua historia. Alisema kwa kuwa kuna uelewa mdogo kwa Watanzania juu ya jambo hilo huku wengine wakijipenyeza na kuingia ni bora ofisi ya Bunge ikatoa elimu.

0 Response to "HIVI NI KWELI MWENGE WA UHURU UNACHOCHEA MAAMBUKIZI YA UKIMWI?"

Post a Comment