WAHITIMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU | JIFUNZE UJASIRIAMALI

WAHITIMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU

WAHITIMU wa vyuo vikuu nchini wametakiwa kuwa wabunifu ili kuhakikisha elimu waliyoipata inabadilisha maisha yao na jamii kwa ujumla.

Wito huo ulitolewa juzi na Katibu Tawala wa Wilaya ya Tanga, Bernard Maselina,  kwenye mahafali  ya kwanza ya Chuo Kikuu cha Eckenford mkoani hapa.
Alisema wahitumu hao wanapaswa kuhakikisha elimu waliyoipata inawasaidia kutatua mambo ya msingi na kuwa chachu ya mabadiliko katika vijiji vyao, mkoa na taifa kwa ujumla.
“Tunajua  ugumu wa shule, hongereni kwa kumaliza. Mkakitangaze vema chuo hiki kwani sitarajii kumuona mhitimu akizurura mitaani,” alisema Katibu Tawala.
Mmiliki wa chuo taasisi ya Eckenford, Remens Tarimo, aliwaasa wahitimu hao kuitumia vema elimu hiyo na kuhakikisha inakuwa mkombozi wa maisha yao kwa kuwa wabunifu katika kila nyanja.
Akizungumza kwa niaba ya wahitimu hao, Agness Mushi, alisema wanaahidi  kuwa wazalendo na waadilifu katika kuitumikia nchi kwa kupitia elimu waliyoipata na kuahidi kuwa watakitangaza vema chuo hicho.
Jumla ya wahitimu 327 katika ngazi ya shahada, Stashahada na Astashahada wamehitimu katika chuo hicho.
CHANZO: Tanzania Daima.


0 Response to "WAHITIMU WATAKIWA KUWA WABUNIFU"

Post a Comment