KWANI HIZI SIYO DAWA ZA KUKUZA KUKU HARAKA? PREMIX, LYSEN, BOOSTER, COCCIDIOSTAT NA DCP | JIFUNZE UJASIRIAMALI

KWANI HIZI SIYO DAWA ZA KUKUZA KUKU HARAKA? PREMIX, LYSEN, BOOSTER, COCCIDIOSTAT NA DCP

EGG BOOSTER

Kawenye mfululizo wa makala za MSIMU WA KUKU leo tutajibu swali la msomaji wetu mmoja aliyeuliza hivi;


Habari mtaalam, Naitwa Amos...nipo Njombe.

Nimesoma makala zenu za msimu wa kuku zimenivutia, lakini kuna kitu bado kinanichanganya sijakielewa vizuri.

Mnadai kuku huwa hawapewi kabisa madawa ya kuwakuza haraka wala kuwafanya watage mayai mengi, lakini nimewahi kusoma sehemu nyingi nikaona kuku hupewa dawa na vitu vingi sana mbali na chakula na antibiotics za kutibu magojwa, miongoni mwa hivyo vitu nitavitaja hapa;

               (1)     Premix

               (2)     Egg Booster

               (3)     Coccidiostat

               (4)     Vitalyt

               (5)     DCP

               (6)     Threonine

               (7)     Lysine

               (8)     Methionine

               (9)     Mycotoxin binder

Naomba unifafanulie vizuri ikiwa kama hizo zote siyo madawa yenyewe na Homoni za kuboost  kuku wakue upesi ni kitu gani?

Amos

 

MAJIBU:

Asante sana ndugu Amosi kwa swali lako;

Ni kweli katika tasnia ya ufugaji wa kuku hasa kuku wale wa kisasa wakiwemo, kuku wa nyama broile, kuku wa mayai layers na hata kuku chotara kama kuroiler, Sasso na wengineo kuna dawa na virutubishi mbalimbali (Additives) vinavyoongezwa katika chakula chao ili waweze kuwa na afya njema.

Vitu hivyo ama Additives ni tofauti kabisa na homoni za ukuaji (growth hormones) zinazopigiwa kelele sana na watu kote duniani, vimeidhinishwa na mashirika mbalimbali yanayoshugulika na afya duniani yakiwemo yale ya Umoja wa Mataifa yenyewe.

Vitu vyote ulivyovitaja hapo juu na vingine ambavyo hukuvitaja lakini vinatumiwa na wafugaji wa kuku tunaweza kuviweka katika makundi makuu 4 kama ifuatavyo;

                         (1)     Vitamini

                         (2)     Madini

                         (3)     Amino acids (Protini)

                         (4)     Dawa na Chanjo

Vitu hivi havina sthari yeyote ile mbaya kwa kuku wenyewe wala kwa binadamu wanaokula kuku ikiwa tu vitatumika kama ilivyopendekezwa na wataalamu wa mifugo. Hata ikiwa hautawapa kabisa kuku wako vitu hivi, kuku hao watavipata kwenyo mlo wa kawaida wanaokula kila siku na endapo watavikosa basi matokeo yake hudumaa au kupatwa na magonjwa mbalimbali.

Kwahiyo vyote ni virutubisho vinavyopatikana kwenye udongo au kwenye mimea wakati kuku akijitafutia chakula chake kiasili kwa kuchakurachakura mchangani. Wataalamu wamevitengeneza makusudi kutokana na kuku wa kisasa kuwa hawana uwezo wa kujitafutia vyakula wenyewe na hata wangeweza haiwezekani kutokana na kuku hao kufugwa idadi kubwa mno ya kuku kibiashara

Hapa chini nitaelezea kimoja kimoja baada ya kuvipanga kwenye makundi yake kwenye jdwali;

VITAMINI

Premix, Egg Booster, Vitalyt, nk.

MADINI

DCP, Chokaa nk,

PROTINI

Threonine, Lysine, Methionine, Tryptophan nk.

 

DAWA & CHANJO

Mycotoxin binder, Antibiotics, Coccidiostat nk.

 

 

Premix,

Hili ni neno na lina maanisha kitu kinachoongezewa baada ya kingine. Ni mchanganyiko wa Vitamini za aina mbalimbali na madini kwa ajili ya kuongeza kwenye chakula cha kuku. Zipo za aina tofauti kulingana na umri wa kuku au kundi mfano wanaotaga, vifaranga, wa nyama nk.

Egg Booster

Kama ilivyokuwa kwa premix hapo juu hii nayo ni mchanganyiko wa vitamin mbalimbali na madini kwa ajili ya kuku wanaotaga, Neno Booster lisikutishe, madini na vitamin husaidia mwili kutengeneza protini za kukuza mwili

Vitalyt

Pia nayo ni mchanganyiko wa Vitamini kwa ajili ya mifugo

DCP

Kirefu chake ni Dicalcium Phosphate: Huu ni mchanganyiko wa madini ya Calciun na Phosphate kwa ajili ya kuimarisha mifupa ya kuku

Chokaa

Nayo pia ni madini na hupatikana hata kwenye mifupa ya wanyama, viumbe wa bahari, konokono nk.

Threonine, Lysine, Methionine, Tryptophan

Hizi ni amino acids au Protini ambazo hupatikana kwenye vyakula mbalimbali na hata binadamu pia tunazihitaji sana kwa ajili ya ufanyaji kazi mzuri wa tishu na seli za mwili. Hazina madhara yeyote kwani hata usipowawekea kuku kwenye chakula watazipata wenyewe kwenye kile watakachokula, wakikosa kabisa watadhoofika na kuugua.

Coccidiostat, Mycotoxin binder, Antibiotics nk.

Hili ni kundi la dawa, ka mfano hii Coccidiostat huongezwa kwenye chakula cha kuku kuzuia ugonjwa wa coccidiosis unaosababishwa na protozoa.

Mycotoxin binder ni kiua sumu pia kinachozuia sumusumu zinazotokana na chakula

Kwenye vyakula vya kuku zinaweza zikaongezwa additives nyingine zozote zile ilimradi tu zimeidhinishwa na mamlaka zinazosimamia mifugo au serikali.

Antbiotics: Kwa upande wa antibiotiki au madawa ya kutibu magojwa ya bacteria ndio penye tatizo kubwa kushinda hata dhana nyingine zote watu wanazohofia.

Matumizi ya dawa hizi hayakatazwi kwa kuku wanaoumwa lakini tatizo kubwa lipo kwa wafugaji hasa wale wakubwa na hata wadogo, wanapoamua kuzitumia dawa hizi kama kinga ya magonjwa hayo au kuzitumia kiholela pasipo kuzingatia kwamba dawa hizihizi zina asili moja na zile tunazotumia wenyewe binadamu.

Matokeo ya matumizi hayo holela husababisha usugu mkubwa wa dawa hizo kwa walaji wa kuku waliozoeshwa hayo madawa. Hili ni tatizo kubwa linalosumbua siyo Tanzania tu bali dunia nzima.


...............................................

Mpenzi msomaji wa makala hii, Katika MSIMU WETU WA KUKU, hii ni makala ya 5 katika mfululizo wa maudhui yanayohusiana na kuku. Unaweza kujisomea makala nyingine 4 chini ya makala hii.

Leo pia ni siku ya 3 ya Semia ya kuandika Mchanganuo wa kuku Kuroiler wa nyama likiwa ni Darasa la awamu ya 3. Katika siku hii tunakwenda kujifunza vipengele vya;  SOKO, MIKAKATI & UTEKELEZAJI

Unaweza kujiunga na semina hata ikiwa umechelewa kwani tuna utaratibu wa kuwafundisha wale wote waliochelewa kabla ya muda rasmi wa darasa. Darasa huanza rasmi saa 3 kamili usiku

Kujiunga na Semina hii, lipia shilingi 10,000/= kupitia namba zetu 0712202244 au 0765553030 Peter Augustino Tarimo, kwa ajili ya kupata Kitabu na Mchanganuo kamili wa kuku 300 wa kuroiler. Vitu hivi ni muhimu kwa ajili ya kufanya rejea.

Ukishalipia tuma ujumbe; “NATAKA SEMINA YA KUROILER NA OFFA YA VITU 9

Baada ya hapo nakutumia papo hapo Kitabu, mchanganuo wako wa kuroiler pamoja na OFFA ya michanganuo mingine 6 jumla vinakuwa vitu 9

 

OFFA HIYO NI HII HAPA CHINI;

 

1.    Kitabu: MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI (Page 430)

2.    Mchanganuo Mpya: Biashara ya ufugaji wa kuku chotara wa nyama 300 (Chotara Poultry Production Co.)

3.    Mchanganuo wa kuku wa nyama (Tumaini Broilers)-kiingereza

4.    Mchanganuo wa kuku wa nyama (Tumaini) -kiswahili

5.    Mchangauo wa kuku wa mayai (Mayai Bora Project)-kiswahili

6.    Mchanganuo wa Matikiti maji (Kibada watermelon)-kiswahili

7.    Mchanganuo wa Mgahawa wa chakula (Jane Restaurant)-kiingereza

8.    Mchanganuo wa Mgahawa wa chakula (Jane Restaurant) –kiswahili

9.    Kuujiunga Mastermind group (Option/hiyari)

 

 

 

 



SOMA NA HIZI HAPA:

                 1.                Hydroponic fodder: jinsi ya kuotesha majani ya mifugo katika trei za aluminium na plastiki bila udongo

                 2.                Njia mpya za kufanya mambo: dunia, biashara, ajira vinabadilika kwa kasi ya ajabu

                 3.                Kuku wa kienyeji hubadilisha chakula kuwa nyama polepole zaidi kuliko kuku wa kisasa (high feed conversion ratio)

                 4.                Hatua kwa hatua jinsi ya kuandika mchanganuo wa biashara ya kuku wa nyama 2000 kuomba mkopo taasisi za fedha

                 5.                Muongozo kamili wa jinsi ya kufuga kuku wa nyama (broilers) kitaalamu - semina siku-3

          

0 Response to "KWANI HIZI SIYO DAWA ZA KUKUZA KUKU HARAKA? PREMIX, LYSEN, BOOSTER, COCCIDIOSTAT NA DCP"

Post a Comment