SEMINA SEHEMU YA 3: MPANGO WA BIASHARA, UFUGAJI KUKU WA NYAMA KUROILER – (SOKO, MIKAKATI & UTEKELEZAJI) | JIFUNZE UJASIRIAMALI

SEMINA SEHEMU YA 3: MPANGO WA BIASHARA, UFUGAJI KUKU WA NYAMA KUROILER – (SOKO, MIKAKATI & UTEKELEZAJI)

Uendeshaji kuku wa nyama kroiler

SEMINA KUROILER SEHEMU YA 3:

(SOKO, MIKAKATI & UTEKELEZAJI)

 

4.0 Tathmini ya Soko:

Tathmini ya Soko ni sura katika mpango wa biashara inayohitaji taarifa kutoka nje ya biashara husika kuliko sura nyinginezo zote. Taarifa hizo zinahusu hasa wateja watarajiwa, Sekta biashara inapoangukia na Ushindani.

Hii ni kusema kwamba sura hii utatumia sana taarifa ulizozipata wakati wa kufanya utafiti wa soko lako na biashara kwa ujumla.

Kama tulivyokwishaona, utafiti au upembuzi yakinifu kulingana na KITABU CA MICHANGANUO YA BIASHARA NA UJASIRIAMALI unaweza kuufanya kwa njia rahisi kupitia kwenda moja kwa moja kwa wateja wa bidhaa/huduma tarajiwa na kuwauliza maswali mbalimbali yanayolenga kupata taarifa zao na bidhaa wanazonunua. Kitabu hicho kimeeleza njia zote mbili, rahisi na ile ya kitaalamu zaidi ya kutafiti soko la biashara yeyote ile

Utafiti pia unaweza kuufanya kwa njia ya kusoma machapisho au majarida na vyombo vya habari vyenye taarifa kutoka taasisi mbalimbali kama vile Wizara za serikali, Ofisi ya Takwimu ya Taifa, Serikali za mitaa, vyama vya wafanyabiashara na wataalamu wengineo.

Katika mchanganuo wetu huu wa kuku chotara kuroiler tutazingatia baadhi ya vipengele vinavyounda sura hii ingawa siyo lazima tuvitumie vyote kulingana na mahitaji ya biashara yenyewe. Navyo ni; 

4.1 Mgawanyo wa soko

4.2 Soko lengwa

4.2.1 Mahitaji ya soko

4.2.2 Mwelekeo wa soko

4.2.3 Ukuaji wa soko

4.3 Tathmini ya Sekta

4.3.1 Washiriki katika sekta

4.3.2 Usambazaji

4.3.3 Ushindani

4.3.4 Washindani wako wakuu

Kama kawaida wakati nikianza kuandika Sura hii sina budi kuacha nafasi ya kuja kuandika muhtasari wa sura nzima baadae kwa kuchagua baadhi ya mistari au pointi zile muhimu.

4.1 Mgawanyo wa soko

Katika kipengele hiki kidogo nataja ni makundi gani ya soko tutakayoyalenga na nitayataja makundi matatu ambayo ni;

               (1)     .........................................................

               (2)     ..........................................................

               (3)     ..........................................................

Kuligawa soko lako fikiria kwanza ni vigezo vipi vinavyosababisha makundi hayo yatofautiane kwenye kununua mfano umri, kipato, elimu, eneo, ufikiwaji na vyombo vya habari ama kigezo kingine chochote kile. Ikiwa wateja wako ni taasisi au biashara basi unaweza kutumia vigezo kama idadi ya wateja, kiasi cha mtaji, ukubwa wa biashara nk.

Mimi kwa mfano katika makundi haya matatu nimetaja sifa za kila kundi na katika kuligawanya soko hili nimezingatia zaidi idadi ya kuku wanaonunua pamoja na kiasi cha mtaji walichokuwa nacho kama kitofautishi cha makundi hayo.

4.2 Mkakati wa soko lengwa

Hiki ni kipengele kingine kidogo kwenye sura hii ambacho ni kama vile tunazidi kuchambua kile kipengele kilichopita kusudi tupate kipande cha soko tutakachokilenga zaidi ya vingine na kuelezea ni mkakati upi uliotufanya tuchague kulenga zaidi kipande hicho na wala siyo vipande vingine 2.......................

.................Mpenzi msomaji wangu Jipatie mchanganuo kamili wa kuku chotara 300 wa nyama aina ya Kroiler pamoja na Semina yake ya siku 5 uweze kujua undani wa kipengele hiki na vingine ndani ya mpango huu bunifu wa biashara yenye faida kubwa katika kipindi kifupi..............

4.2.1 Mahitaji na Mwelekeo wa soko

Hapa nimeunganisha vipengele vidogo viwili ambavyo ni “mahitaji ya soko” na “Mwelekeo wa soko”, vilipaswa kujitegemea kila kimoja lakini kutokana na ufupi wake nikaona ni vyema niviunganishe pamoja.

Katika kila kipande cha soko unachokilenga unaelezea mahitaji ya wateja katika kipande husika yanayowafanya wanunue bidhaa/huduma zako huku ukilenga zaidi faida aipatayo mteja na wala siyo faida unayoipata wewe.

Kwa mfano sisi hapa hatulengi tu kuwauzia wateja wetu kuku bali tunahakikisha tumekidhi mahitaji ya wateja wetu ya kutaka kitoweo cha kuku kilicho na ladha tamu kwa bei inayohimilika na mtu wa kipato chochote, vilevile ni kukidhi hitaji la wateja la kula nyama nyeupe inayosisitizwa sana na wataalamu wa afya likiwemo Shirika la chakula Duniani FAO

Kwenye Mweleko wa soko unataja kigezo kinachoonekana kubadilisha hali ya soko siku za usoni, kwa mfano sisi hapa katika mchanganuo wetu huu mwelekeo wa soko la kuku jijini Dar es salaam unaonyesha wateja.............................................. ..........................................................................................................................................................................................................

4.2.2 Ukuaji wa Soko

Kulingana na utafiti wako wa soko ulioufanya, hapa unatakiwa kutoa nukuu kulingana na taarifa mbalimbali za kitaalamu ulizozipata kuonyesha ni jinsi gani soko lako lina uwezekano wa kukua.

Kwa mfano kwenye mchanganuo wetu huu nilionyesha soko kukua kwa kutumia takwimu za Sensa ya watu na makazi, kwamba kila mwaka idadi ya wateja jijinI Dar es salaam wanaohitaji kitoweo cha kuku huongezeka kwa sababu idadi ya watu nayo inaonyesha kukua....................................................

Ningeliweza pia kwa mfano kutumia taarifa za wataalamu wengine kwenye sekta hii ya kuku zinazoonyesha ukuaji wa soko hili mwaka hadi mwaka kama vile mauzo ya kuku katika soko moja moja, idadi ya kuku wanaochinjwa kwa mwezi, idadi ya machinjio zinavyoongezeka kila mwaka nk.

4.3 Sekta ya Ufugaji wa kuku (Ndege)

Katika tathmini ya sekta uliyopo, kwanza unataja ni sekta gani hiyo, kwa mfano sisi hapa tumetaja ni sekta ya ufugaji wa kuku/ndege, unaweza ukataja ndege au kuku vyote ni sawa. Kama ilivyokuwa kwa taarifa za soko, Sekta nayo taarifa zake hutokana na utafiti ulioufanya hasa kutokana na machapisho mbalimbali yanayohusiana na sekta ya kuku.

Taarifa hizo mbali na zile zinazohusisha kampuni/biashara yako moja kwa moja lakini pia unatakiwa kuwa na taarifa zinazohusu mazingira mazima yanayoizunguka biashara hiyo

Unaweza kuzungumzia jambo lolote lile kwenye sekta linaloshika chati (kutrend) kwa wakati huo huku ukitoa takwimu mbalimbali ulizonukuu kutoka katika utafiti wako. Kwa mfano kwenye mchanganuo wetu huu wa kuku wa Kuroiler kwa ajili ya nyama kwenye sekta nimezungumzia......................................... ...............................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Vilevile nilieleza jinsi sekta hiyo ilivyogawanyika makundi makundi pamoja na washiriki wake mbalimbali wanaounda sekta nzima.

4.3.1 Ushindani

Hiki ni kipengele kidogo ndani ya Sekta. Unaweza ukaona kwamba sijaweka katika mchanganuo huu vipengele vidogo vyote kama vilivyotajwa kwenye mlolongo wa vipengele kamili kwani siyo lazima mtu kufanya hivyo. Mfano sijaweka, “Washiriki katika sekta” na “Mfumo wa usambazaji

Hivyo niliingia moja kwa moja kwenye kpengele kidogo cha Ushindani nikaelezea hali ya ushindani ilivyo, kwamba ushindani katika biashara ya kuroiler siyo mkubwa sana katika eneo la Kimara ingawa wapo washindani wasiokuwa wa moja kwa moja. Nilielezea na aina mbili za ushindani, ule wa moja kwa moja na usiokuwa wa moja kwa moja.

Ningleliweza pia kuelezea na kigezo kinachotumika wateja kuchagua ni kwa mshindani yupi wanunue kutoka kwake mfano wanaweza kutumia kigezo cha bei, ubora wa huduma, jina (brand) ama kigezo kingine chochote kile. 

Kipengele hiki pia nilikiunganisha na kipengele kingine cha “Washindani wako wakubwa” ambacho kilipaswa kuwa kinajitegemea baada ya hiki.

Kwa kila mshindani niliyemtaja nimeelezea sifa zake, nguvu na udhaifu aliokuwa nao katika vigezo/maeneo mbalimbali mfano bei, hali ya kifedha, teknolojia, jina, usambazaji nk.

Mazingira ya Biashara

Nilisema haipaswi kukariri mlolongo wa vipengele kama ulivyotajwa bali unautumia tu kama muongozo. Ndio maana unaweza kuona kipengele hiki hakipo kwenye mlomlongo rasmi nilioweka pale juu lakini nimekiweka kwenye mchanganuo na inategemewa mtu unaweza ukaweka kipengele kingine chochote ilimradi kihusiane na soko.

Mfano hapa niliweka vipengele vidogo vya “Mazingira ya nje ya biashara (PESTLE)” na “NUFUVI”, kwa kirefu (Nguvu Udhaifu, Fursa na Vikwazo)

Tathmini hizi 2 kwa ujumla zinaelezea mazingira ya biashara au nguvu mbalimbali kutokea nje na ndani ya biashara yenyewe zinazoweza kuiathiri biashara yako katika mlengo chanya au hasi. Faida zake ni kwamba zinakuwezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali kwa urahisi zaidi na kuzitumia fursa zilizopo kikamilifu.

4.4 Mazingira ya nje ya Biashara (PESTLE)

Kirefu cha PESTLE kwa kiingereza ni Political, Economoc, Social, Technological, Legal and Enviromental. Ikimanisha, mazingira ya Kisiasa, Kiuchumi, Kijamii, Kiteknolojia, Kisheria na Kimazingira. Vyote nimevielezea vizuri kabisa kwenye mpango wa biashara hii ya ufugaji wa kuku chotara wa nyama kroiler.

4.5 Nguvu, Udhaifu, Fursa na Vikwazo (NUFUVI au SWOT analysis kwa kiingereza)

Kama ilivyokuwa kwa mazingira ya nje ya biashara hapo juu, hii nayo ni tathmini lakini yenyewe imebeba mazingira ya ndani ya biashara na mazingira ya nje ya biashara kwa pamoja.

Nguvu na Udhaifu ni mazingira chanya na hasi ya ndani ya biashara wakati Fursa na Vikwazo ni mazingira ya nje ya biashara chanya na hasi. Chanya namaanisha mazingira wezeshi na hasi ni mazingira yale yanayodhoofisha biashara au kukwamisha biashara isishamiri.

Mwisho wa kipengele cha Soko, karibu kipengele cha Mikakati na Utekelezaji

 

5.0 Mikakati na utekelezaji

Mikakati ni malengo au vipaumbele vya biashara ulivyochagua miongoni mwa vitu vingine ili kuifanya iweze kuwa juu kuliko za washindani wako.

Tuseme labda umelenga kuwa na mauzo ya shilingi milioni 10 kwa mwezi katika biashara yako, ni lazima ukae chini na kupanga utaitangaza vipi biashara yako, utauza namna gani na hata usambazaji utakuwa vipi ikiwa ni bidhaa nk.

Ili kuielewa vizuri sura hii na nyinginezo ni vyema ukawa nacho kitabu chako cha Michanganuo ya Biashara na Ujasiriamali pamoja na mchanganuo kamili wa Biashara hii ya kuku wa nyama Kuroiler.

Kabla ya kufanya chochote kwenye Sura hii hebu kwanza tuweke mezani vipengele vidogo vinavyounda sura hii nzima kama dira itakayotuongoza;

5.1 Nguvu za kiushindani

5.2 Mkakati wa Soko

5.2.1 Kaulimbiu ya kujipanga katika soko

5.2.2 Mkakati wa Bei

5.2.3 Matangazo na Promosheni

5.2.4 Programu za masoko

5.3 Mkakati wa Mauzo

5.3.1 Makisio ya mauzo

5.3.2 Programu za mauzo

5.4 Mkakati wa ushirkiano

5.5 Vitendo na Utekelezaji

Mwanzoni kabisa nimeweka ufupisho wa vipengele vya sura hii nzima ambao niliandika mwishoni baada ya kukamilisha sura nzima

5.1 Faida za kiushindani

Hivi ni vitu biashara/kampuni inavyofanya vizuri kuzidi washindani wake na hivyo kujitofautisha nao, na hapa nimevitaja vitu 3 visome kwenye mchanganuo wako wa kuku kuroiler wa nyama

5.2 Mkakati wa Soko

Mkakati wa soko chini yake umebeba vipengele vidogo kadhaa ambavyo ni bidhaa, Bei, Matangazo & Promosheni na Usambazaji, kwahiyo hapa tunaweka muhtasari tu wa vipengele hivyo kisha tunaendelea na vipengele vyenyewe

5.2.1 Bidhaa

Hapa nimeelezea mkakati wetu wa bidhaa jinsi CPPC tutakavyozalisha.......................................................................... .....................................................................................................

5.2.2 Matangazo & Promosheni

Ni mkakati wa kuhakikisha wateja wetu watarajiwa wanapata taarifa za uwepo wa bidhaa zetu na kuvutiwa nazo, na nimeelezea katika mchanganuo wetu ni mambo gani tutakayoyafanya kutimiza hilo

5.2.3 Bei

Nimeelezea pia ni mkakati upi kwenye suala la upangaji wa bei tutakaoutumia tofauti na washindani wetu ili kuweza kuibuka kidedea sokoni. Fungua mchanganuo wako wa ufugaji wa kuku chotara wa Kroiler usome mkakati huo mpaka mwisho

5.3 Usambazaji

Mkakati wa usambazaji nimetaja njia zitakazotumika kuwafikishia wateja kuku nikataja................................................ ..........................................................................................................................................................................................................

5.3 Mkakati wa Mauzo

Mauzo ni mkakati tofauti na ile ya Soko tuliyoiona hapo juu na chini yake umebeba pia mikakati mingine midogomidogo kama Makisio ya mauzo na Programu za mauzo. Nimeweka maelezo ya ni kipi kitakachofanyika kuhakikisha mauzo yanakuwa makubwa na kwa ufanisi zaidi

5.3.1 Makiso ya mauzo

Hapa nimekisia mauzo kwa kila bidhaa yatakuwa shilingi ngapi kwenye mzunguko mmoja wa wiki 12 kisha mwaka 1 na miaka 2 inayofuata unaweza kucheki kwenye mchanganuo kamili wa kuku chotara wa nyama kuroiler

5.4 Utekelezaji

Baada ya kuweka mikakati mbalimbali hapa ndipo unapoonyesha mikakati hiyo utakavyoitekeleza. Nimechora jedwali linaloonyesha.................................................................. ..........................................................................................................................................................................................................

 

Mpaka hapo tumemaliza Sehemu yetu ya tatu ambapo tulichanganua Sura mbili za Soko na Mikakati & Utekelezaji. Karibu Sehemu ya nne


SEMINA SEHEMU YA 2                    SEMINA SEHEMU YA 4




SOMA NA HIZI HAPA;

1.   Hydroponic fodder: jinsi ya kuotesha majani ya mifugo katika trei za aluminium na plastiki bila udongo

2.   Kupata faida kwenye ufugaji wa kuku wa kienyeji au wa kisasa mfugaji mjanja hutumia mbinu hizi.

3.   Ufugaji wa kuku wa kisasa wa mayai vs kuku wa nyama ni biashara ipi inayolipa faida zaidi?

4.   Njia mpya za kufanya mambo: dunia, biashara, ajira vinabadilika kwa kasi ya ajabu

5.   Gharama za ujenzi wa banda la kuku 100 chotara au kienyeji ni shilingi ngapi?

6.   Mwaka wa ubunifu zaidi kwenye biashara kukabiliana na majanga

 

0 Response to "SEMINA SEHEMU YA 3: MPANGO WA BIASHARA, UFUGAJI KUKU WA NYAMA KUROILER – (SOKO, MIKAKATI & UTEKELEZAJI)"

Post a Comment