ETI NI KWELI BIASHARA YA GENGE LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA INA FAIDA NUSU KWA NUSU? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

ETI NI KWELI BIASHARA YA GENGE LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA INA FAIDA NUSU KWA NUSU?

genge la matunda na mbogamboga

Swali hili ikiwa kama biashara ya genge la matunda na mbogamboga ina faida nusu kwa nusu nimekuwa nikikutana nalo mara nyingi lakini nikawa nakwepa kulijibu moja kwa moja kutokana na sababu kubwa kwamba sikuwa nimewahi kufanya utafiti wa kina kuhusiana na biashara hii. 

Watu huhusianisha au kuifananisha biashara ya genge na biashara nyingine ya duka la rejareja ambayo tayari nilikwishaifanyia utafiti na kuandika kitabu chake siku za nyuma. Kiukweli ijapokuwa biashara hizi mbili genge na duka zote ni biashara za rejareja na zina mambo mengi ya kufanana lakini pia zina tofauti kadhaa

Mmoja kati ya waliowahi kuniuliza swali hili ni Bwana Jackson wa Tegeta jijini Dar es salaam aliyeuliza kama ifuatavyo kupitia mtandao wa watsap;

“Mtaalamu nimekuwa nikifuatilia sana makala zako kuhusu biashara ya duka la rejareja lakini mimi nataka nianze kwanza na genge la matunda na mbogamboga shauri ya mtaji nilio nao kuwa kidogo mno, sasa ningependa kufahamu, hivi eti biashara ya genge faida yake ni nusu kwa nusu ukinunua kitu shilingi 100 unakwenda kupata faida shilingi 100 juu yake?”  

Swali hili lilinisukuma kuanza kufanya utafiti mkubwa kuhusiana na biashara hii ya genge la matunda na mbogamboga kwani kama nilivyotangulia kusema ni biashara inayoshabihiana na ile ya duka la rejareja ambayo tayari nazielewa ‘ABS’ zake

Mimi naishi Mbezi ya Kimara jijii Dar es salaam hivyo nilianzia hapahapa Mbezi Temboni jirani kidogo na stendi ya mabasi. Nikamtafuta mmiliki mmoja wa genge la matunda na mbogamboga nikajenga naye ukaribu ulioniwezesha kuijua biashara hii kwa undani kabisa.

Mmiliki wa genge hili huchukua bidhaa zake hasahasa katika soko la Mabibo lililopo karibu na Manzese lakini pia mara chache huenda masoko ya Mbezi mwisho, Buguruni na Temeke Sterio kwa baadhi ya bidhaa. Kwahiyo siku moja nikaongozana naye moja kwa moja mpaka Mahakama ya ndizi Mabibo, soko lililopo jirani na kituo cha daladala cha Big Brother

Alinionyesha jinsi wanavyonunua bidhaa, nikatafiti bei za matunda na mbogamboga pamoja na kufanya kila kitu nilichohitaji kufanya katika ule utafiti wangu. Kwa kweli nilizifahamu siri nyingi sana za biashara ya genge ambazo kukosa kufanya utafiti huu nisingeliweza kamwe kuzifahamu.

MAJIBU:

Ndugu yangu Jackson, mtu asikudanganye kuwa eti biashara ya genge la matunda na mbogamboga bidhaa zake zote zina faida nusu kwa nusu hapana, isipokuwa tu ni kweli kwa ujumla bidhaa za genge faida yake ni kubwa kidogo ukilinganisha na bidhaa kwenye biashara ya duka la rejareja.

Ni ukweli usiopingika kwamba kuna baadhi ya bidhaa za genge(chache) ukiuza unapata shilingi kwa shilingi nikimaanisha faida ni nusu kwa nusu lakini siyo zote na utakapotafuta wastani utakuta kwa biashara nzima(bidhaa zote kwa pamoja) faida haiwezi ikawa nusu kwa nusu shauri ya bidhaa nyingine nyingi faida yake kuwa chini.

Kwenye duka la rejareja kwa mfano imethibitishwa kwamba wastani wa faida ghafi kwa mauzo ya bidhaa ni asilimia 25% - 30% maana yake kwa kila mauzo ya shilingi 100 unapata faida wastani wa shilingi 25 mpaka 30

Katika utafiti wangu nilioufanya Temboni asilimia ya faidaghafi kwenye mauzo ya bidhaa za genge kwa wastani nilikuta ni asilimia 30%  mpaka asilimia 35%. Hii inamaanisha kwamba katika kila mauzo ya shilingi 100 faida ghafi ni wastani wa shilingi 30 mpaka 35. Kumbuka faida ghafi maana yake ni faida kabla hujatoa gharama za kudumu za uendeshaji, kodi na riba.

Huu ni utafiti nilioufanya mwenyewe binafsi na si wa kusoma mahali. Katika mfululizo wa makala zangu hizi maalumu kwa ajili ya genge nitakuja kuelezea kwa mifano halisi jinsi nilivyokokotoa hii asilimia 30% mpaka 35% kama faida ghafi

Katika makala hizo zijazo pia nitazitaja baadhi ya bidhaa za genge ambazo unapozinunua sokoni unakwenda kupata faida pasu kwa pasu nikimaanisha faida ni nusu kwa nusu ama ukinunua shilingi mia unakwenda kuiuza mia mbili, hivyo usikose kufuatilia blogu yako hii ya jifunzeujasiriamali kila siku msimu huu wa genge la matunda na mboga.  

Ijapokuwa nimesema kwenye genge kuna baadhi ya bidhaa unapata faida nusu kwa nusu lakini haimaanishi kwamba faida ya genge zima kwa wastani ni nusu kwa nusu pia hapana, kuna bidhaa nyingine nyingi zina faida kidogo na hivyo kusababisha wastani wa faidaghafi nzima ya genge kuwa hiyo asilimia 30% mpaka 35%

Sababu kubwa inayofaya iwe vigumu kuuza kila bidhaa ya genge kwa bei mara mbili ya ile uliyonunulia ili faida ghafi iwe nusu kwa nusu ni ushindani mkali. Wakati wewe unanunua papai shilingi elfu moja kwa bei ya jumla na kutaka kwenda kuliuza shilingi elfu mbili kwa bei ya rejareja ili upate faida nusu kwa nusu, mshindani wako pembeni mwenye genge kama lakwako yeye anauza papai kama hilohilo kwa shilingi 1,500/= pekee

Utaona yakwamba mshindani wako huyu atauza na wewe mapapai yako yatakudodea hutapata wa kumuuzia ng’o, na utalazimika tu hatimae na wewe kuuza shilingi 1,500 au vinginevyo basi chini ya hapo kusudi uweze kwenda na hali halisi ya soko lilivyo

Biashara za rejareja kwa ujumla huwezi ukaweka kiasi kikubwa sana cha faida kufikia nusu kwa nusu faida, tazama bishara mfano Supermarkets huwa wanaweka faida kidogo sana mpaka wakati mwingine kufikia hata asilimia 1% ya faida halisi kwa mauzo (profit margin), baada ya kutoa gharama zote. Lakini wanachojivunia zaidi wao ni mauzo mengi (mass sales).

Ukiuza kwa wingi sana hata kama unapata faida kidogo sana kwa kila bidhaa hamna tatizo kwani ile faida kidogokidogo ikilundikana inakuwa kubwa haraka, na supermarket kwa kuwa wana bidhaa nyingi mchanganyiko hii  faida ya asilimia 1% inawatosha kwani kwa siku ni mamilioni ya shilingi

Ripoti kamili ya utafiti wa biashara ya genge la matunda na mbogamboga

Ripoti nzima ya utafiti wangu huu wa biashara ya genge la matunda na mbogamboga ipo tayari na nimeiweka ndani ya kitabu cha BIASHARA YA GENGE LA MATUNDA & MBOGAMBOGA.

Kama kawaida hatujaacha kitu chcohcote ni Ripoti kamili. Ikiwa unataka kuanzisha genge au tayari unalo tafadhali usiache kujipatia madini haya adimu utakuja nishukuru baadae

Kitabu hiki kipya cha Biashara ya Genge la Matunda na Mbogamboga bei yake ni shilingi 5,000/= nakala tete (Softcopy) wakati kile cha Duka la rejareja bado ni shilingi 6,000/=

Vitabu hivi viwili siyo kwa walio na duka au genge tu hapana, vinafaa hata kwa yule anayefanya biashara nyingne yeyote ile ya rejareja.

Vitabu hivi 2 kwa ajili ya biashara za rejareja unaweza kujipatia kwa urahisi muda wowote kwenye simu au kompyuta yako kwa kufanya malipo kupitia nambari 0712202244 Peter Augustino Tarimo, kisha nitumie ujumbe wa sms kwa namba hiyohiyo au watsap kwa namba, 0765553030 na nitakurushia kitabu/vitabu vyako muda huohuo

AU

Unaweza pia kununua vitabu vyako moja kwa moja bila hata ya kuwasiliana na sisi katika duka letu la mtandaoni la Selar kwa kutumia viungo vifuatavyo hapo chini; (Bonyeza kulipia moja kwa moja kwa kutumia mtandao wako wa simu, Tigo(Yas), Voda au Airtel:)


                           1.   BIASHARA YA GENGE LA MATUNDA & MBOGAMBOGA 2025: BEI = 5,000/=


                           2.    DUKA LA REJAREJA TOLEO JIPYA 2024 : BEI = 6,000/=

                       

NAKALA NGUMU (HARDCOPY) YA KITABU CHA  GENGE LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA 2025 TUNAKULETEA MPAKA ULIPO DAR ES SALAAM KWA SH. 25,000/=. UNAPATA BURE NA KITABU CHA DUKA LA REJAREJA

PIA UNAPONUNUA KITABU CHA DUKA LA REJAREJA NAKALA NGUMU (HARDCOPY) SH.25,000/= TUNAKUPATIA NA KITABU CHA GENGE BURE BILA MALIPPO

MIKOA MINGINE PAMOJA NA ADA YA BASI NI SH. 30,000/=

.......................................

Karibu ufanye mapinduzi makubwa kwenye biashara yako ya rejareja mwaka huu wa 2025 haijalishi ni duka la vyakula, nguo, dawa, genge au tu unauza ubuyu wako kwenye meza sokoni.”

Peter A. Tarimo

0712202244 / 0765553030



SOMA NA HIZI HAPA;

Mchanganuo wa biashara ya genge la kisasa la matunda, mbogamboga na vyakula

Siri ya kufanikiwa biashara ya kuuza vinywaji baridi vyenye faida ndogondogo

Biashara ya mtaji wa million mbili (2) ninayoweza kufanya ni ipi? naomba msaada

Biashara bunifu za mtaji mdogo zinavvyoweza kukutoa kimaisha mwaka huu

Orodha ya biashara za vijijini unazoweza kuanza na mtaji wa sh. laki 3 (300,000/=)

 

0 Response to "ETI NI KWELI BIASHARA YA GENGE LA MATUNDA NA MBOGAMBOGA INA FAIDA NUSU KWA NUSU?"

Post a Comment