MALENGO YAKO KIFEDHA 2025, JE UNAYATIMIZA KAMA ULIVYOYAPANGA JANUARI IKIWA NI ZAIDI YA ROBO MWAKA SASA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MALENGO YAKO KIFEDHA 2025, JE UNAYATIMIZA KAMA ULIVYOYAPANGA JANUARI IKIWA NI ZAIDI YA ROBO MWAKA SASA?

MALENGO

Huu ni mwezi Aprili katikati kuelekea Mei lakini siyo ajabu kukuta idadi kubwa ya watu waliokuwa na shamrashamra za kujiwekea malengo kadha wa kadha ya kifedha pale Januari wameshasahau ama kuachana na malengo hayo kitambo

Binafsi mimi ni mhanga mara kwa mara wa malengo ya Januari lakini kila wakati nimekuwa nikijitahidi kurekebisha makosa na safari hii nikaja kugundua njia yenye nguvu sana ya kujiepusha na tabia ya kuachana na malengo ya maisha niliyojiwekea Januari kabla hata ya miezi mitatu ya kwanza (Robo ya mwaka) kumalizika.

Somo hili ni moja kati ya mfululizo wa masomo mengine mengi yaliyo na maudhui yahusuyo mzunguko wa fedha kwenye Mastermind Group la Michanganuo-online kila siku.

Kwa kipindi kirefu watu wamekuwa na mitazamo tofauti kuhusu suala la uwekaji wa malengo ya mwaka hususani malengo yale ya kifedha ya muda mrefu mfano malengo ya mwaka, miaka 2, miaka 5 na wakati mwingine hata malengo ya Milenia.

Ni jambo ambalo limekuwa likiwasumbua watu wengi kutokana na ukweli mchungu kwamba, uwekaji wa malengo ya kifedha au kimaisha ni kitu kimoja na utekelezaji wake ni kitu kingine tofauti kabisa

Katika malengo uliyojiwekea Januari ikiwa hautajifanyia tathmini ya mara kwa mara huku ukirekebisha pale ambapo umetoka nje ya mstari wa malengo yako ni dhahiri kabisa kwamba Desemba itafika na kukukuta hakuna cha maana ulichotimiza.

Nimegundua kwamba unapokuwa na lengo kubwa ulilojiwekea na litakalochukua muda mrefu kulitimiza tuseme labda miezi, mwaka nk. adui namba moja atakayekuzuia usilitimize ni wasiwasi, ile hali ya kuwa na mashakamashaka.

Unajisemea, “Ngoja niache leo nitafanya kesho”, eti ukisubiria mpaka siku utakayokuwa katika ‘mudi’ nzuri ya kulitekeleza au utakapokuwa na hamasa ya kutosha.

Nasema hivyo kwani wataalamu wanakuambia lengo lolote lile kubwa ni lazima ulitimize kidogokidogo kila siku na hili halina ubishi kabisa vinginevyo hautaweza kulitimiza hata ungepewa muda wa karne moja.

Watu mara nyingi tumekuwa tukiingia kwenye mtego wa kukaa tukibweteka na kuanza kuwaza ni kwa jinsi gani tutakavyofurahia (kuenjoy) siku tukitimiza malengo yetu badala ya kuutumia muda huo kufikiria ni nini cha kufanya ili kutimiza malengo tuliyojiwekea kwa uendelevu.

Kwa hiyo msingi mkuu utakaokufanya hatimaye kuyafikia malengo uliyojiwekea Januari ama kipindi kingine chochote kile cha mwaka haijalishi ni lazima iwe uliyaweka mwezi Januari ni mazoea ya kutimiza lengo lako kidogokidogo. 

Katika somo letu hili la leo hivi punde, nitakwenda kukutajia vitu vitano muhimu sana na vilivyokuwa na nguvu (very powerful) ambavyo ikiwa utakwenda kuvitia kwenye matendo basi utaachana kabisa na kilema cha kughairisha utekelezaji wa malengo yako muda mfupi tu baada ya kuyaweka..............

..........................................................................................................................................................................................................................................................................................................................

Ndugu msomaji wangu, somo hili kamili tutajifunza leo kwenye Mastermind group la Michanganuo-online.

Kujiunga na group mwanachama anapaswa kununua kitabu cha Michanganuo ya Biashara & Ujasiriamali ambacho bei yake ni shilingi elfu 10 kwa ajili ya rejea ya masomo mbalimbali atakayojifunza mwaka mzima.

Baada ya kujiunga unaweza kuaccess / kuyapata masomo mengine yote yaliyopita katika channel yetu ya Telegramu pamoja na programu nyingine za kampeni ya  “2025 MAKE YOURSELF GREAT AGAIN”, hivyo unapaswa pia kuwa na account Telegram

 

Mawasiliano:

Watsap/Call: 0765553030

Namba ya kulipia: 0761002125

Peter Augustino

 

Baada ya malipo tuma ujumbe “NIUNGE MASTERMIND GROUP LA MICHANGANUO 2025”

 

 

SOMA NA HIZI PIA:

1.   Maajabu ya kufikiri mambo makubwa na kwanini uweke malengo makubwa maishani

2.   Biashara 7 nzuri za kufanya zitakazokuingizia pesa hata kama umelala.

3.   Ijue falsafa ya kitabu iliyotengeneza matajiri & mabilionea wengi zaidi duniani

4.   Mafanikio na utajiri wa watu wengi umetokana na falsafa hizi 7 za fedha

5.   Shuhuda: wadau waliojipatia offa ya mwisho wa mwaka ya vitabu, michanganuo na kujiunga mastermind group

6.   Wanaofanikiwa maishani wengi husema ‘no’(hapana) kwa vitu hivi 3


0 Response to "MALENGO YAKO KIFEDHA 2025, JE UNAYATIMIZA KAMA ULIVYOYAPANGA JANUARI IKIWA NI ZAIDI YA ROBO MWAKA SASA?"

Post a Comment