NI NINI KULICHOKUWA NYUMA YA HARUSI HII NZURI YA KUPENDEZA? | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NI NINI KULICHOKUWA NYUMA YA HARUSI HII NZURI YA KUPENDEZA?

Harusi ya kupendeza

Ni picha gani inayokujia akilini unaposhuhudia harusi nzuri ya kupendeza kama hii pale Maharusi wakiwa na nyuso zilizojaa tabasamu wanapovishana pete au kulishana keki? 

Kabla ya siku yenyewe ya ndoa kulikuwa na mchakato mrefu kuanzia pale ndugu, jamaa na marafiki toka pande zote mbili, kike & kiumeni walipoanza kukaa vikao vya kupeleka barua, mahari na kuvishana pete ya uchumba.

Kisha vikafuata vikao vya harusi na sendoff sambamba na kuundwa kwa kamati za sherehe ambapo ndugu jamaa na marafiki hapa kila mmoja ‘akapledge’ kile alichofikiri atamudu kuchangia.

Hapa sasa ndipo kiini chenyewe hasa cha sherehe ya harusi kilipo kwani bajeti inaanza kutengenezwa kulingana na kiasi cha fedha kilichokuwa kikitolewa na wadau

kuvishana pete

Mchakato wote huo uliochukua takribani miezi kadhaa unaweza ukauita MIPANGO ya harusi na ndio msingi halisi wa sherehe yeyote ile ya harusi kupendeza.

Ikiwa kama mipango ilikuwa mibovu harusi haitapendeza lakini mipango ikiwa madhubuti na mizuri harusi hufana na watu kufurahia kama hii.

kulishana keki ya harusi

Si harusi tu peke yake bali hata na shughuli nyinginezo karibu zote binadamu tunazofanya ikiwemo BIASHARA, huhitaji mipango au maandalizi kabambe kabla ya matukio yenyewe halisi kufanyika.

Ukitaka biashara yako ishamiri na kukupatia faida kubwa basi huna budi kufanya mipango kabla ya kuianza. Na si unapoanza tu bali hata na biashara ya zamani unaweza pia kuiwekea mpango wa kuifufua au kuifanya iweze kutengeneza faida kubwa zaidi ya ile uliyozoea.

Katika biashara watu wengi tumezoea kupanga tu wenyewe kichwani na kuanza utekelezaji jambo ambalo si baya, lakini kuna kupanga na kisha ukaiweka mipango yako kwenye karatasi jambo ambalo ni zuri zaidi na linalozidisha mara dufu uwezekano wa biashara kufanikiwa kulingana na maelezo ya wataalamu.

Kuandaa mpango wa biashara kuna faida nyingi kubwa ikiwa ni kumfanya mjasiriamali aumize kichwa kuufikiria mchakato mzima wa biashara yake jinsi utakavyokwenda na hivyo kupunguza uwezekano wa kuja kufanya makosa mbalimbali mbele ya safari

Ni sawa na mtu kujifunza biashara yake yote kabla ya kuifanya kwani mpango wa biashara hugusa kila kipengele kinachohusiana na biashara kuanzia wasifu, umiliki, bidhaa/huduma, soko, utawala & wafanyakazi, uendeshaji na fedha.

Kwahiyo ukijua kuandaa mpango wa biashara tayari ‘umehitimu somo la biashara’ maana unakuwa hakuna kipengele kwenye biashara wewe usichokijua. Ndio maana Self Help Books Tanzania chini ya blogu ya jifunzeujasiaramali tukaanzisha mafunzo mahususi kwa ajili hiyo.

Tumefungua Darasa la kujifunza jinsi ya kuandaa mpango/mchanganuo wa biashara yeyote ile bure. Mafunzo haya kupitia group la watsap yanafanyika kila siku sambamba na masomo mengine ya fedha, biashara, ujasiriamali, uchambuzi wa vitabu na ubunifu kwenye biashara.

Unapoingia tu darasani hivi unaanza masomo siku hiyohiyo na unaweza kutumia kiungo kifuatacho kujiunga au kuwasiliana na sisi kwa namba 0765553030 tukuunganishe bure kabisa pamoja na kupatiwa vitabu mbalimbali bila malipo

Karibu ujiunge hapa uanze kujifunza leoleo        

 

https://chat.whatsapp.com/CH2fntry2AbAB71sWhXh5B

 

Peter Tarimo                                            

Mwalimu & Mtaalamu wa Michanganuo ya Biashara

Simu/watsap: 0765553030

0 Response to "NI NINI KULICHOKUWA NYUMA YA HARUSI HII NZURI YA KUPENDEZA?"

Post a Comment